Burudani
Picha: H. Baba na Flora Mvungi wapata mtoto wa kike ‘Tanzanite’
Ndoa ya msanii wa bongo fleva Hamis Ramadhan aka H.Baba na mkewe Flora Mvungi imefanikiwa kupata mtoto wa kike waliyempa jina la ‘TANZANITE’.
Tanzanite
H.Baba ameiambia Bongo5 kuwa mkewe Flora amejifungua salama jana (September 11) majira ya saa 12.30 jioni katika hospitali ya Marie Stopes iliyopo Mwenge.
“Najiskia furaha sana kwasababu hii ndiyo mara ya kwanza naitwa baba, namshkuru sana Mwenyezi Mungu kwa kunipa mtoto wa Kike ambaye tumemuita Tanzanite Hamis, nawashukuru wote pia ambao wametuombea dua” Alisema H.Baba
Bongo 5 inawapa hongera H-Baba na Flora kwa kupata mtoto.