Habari

Picha: Hali ya mtoto Zion aliyepandikizwa mikono ya mtu mwingine inavyoendelea

Mtoto wa mwenye umri wa miaka 10, Zion Harvey ambaye alifanyiwa upasuaji wa upandikizaji wa mikono imeendelea kufanya kazi vizuri.


Kushoto ni picha ya mtoto Zion kabla ya upandikizwaji wa mikono na kulia ikiwa tayari kapandikizwa

Zion alifanyiwa upandikizwaji huo miaka miwili iliyopita baada ya mikono yake kukatwa wakati alipokuwa na umi wa miaka miwili kutokana na ugonjwa wa Sepsis, ambao ni hatari kwa maisha hali iliyofanya madaktari kuamua kuikata mikono hiyo ambayo ilikuwa inakufa.


Mtoto Zion akiwa kabla hayafanyiwa upandikizwaji wa mikono

Kwa sasa mtoto huyo anaweza kuandika, kujilisha, kujivalisha nguo pamoja na kucheza baadhi ya michezo inayotumia mikono.


Zion akifanya mazoezi ya kucheza mpira wa Magongo

Madaktari wapatao 10 na wasaidizi wengine takriban 30 walimfanyia Zion upasuaji usiku wote hadi asubuhi kumpandikiza mikono yake mipya. Wakati huo huo alipokuwa na umri wa maiak minne mtoto huyo aliwekewa figo kutoka kwa mama yake mzazi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents