Michezo
Picha: Hatimaye Alexis Sanchez amejiunga na Arsenal
Mshambuliaji Alexis Sanchez Nyota kutoka Chile mwenye miaka 25 amekamilisha uhamisho wa Pauni Milioni 30 kutoka Barcelona kwenda Arsenal wanaamini atawasaidia ili kuweza kupata ubingwa wa Ligi Kuu ya England
Nyota huyo wa Chile ambaye amesain mkataba wa miaka minne huku kukiwa na kipengele cha kuongeza miezi 12 na mshahara utakuwa paundi laki moja na elfu 40 kwa wiki. Kiwango hicho kitamfanya alipwe sawa na Mjerumani, Mesut Ozil ambaye kwasasa ndiye mchezaji anayelipwa zaidi Emirates.
Maisha mapya: Alexis Sanchez akipozi katika picha akivalia jezi yake ya Asernal kama ishara ya kufungua ukurasa mpya wa maisha ya soka