Habari
Picha: Huyu ndiye aliyeichukua nafasi ya Mr. T Touch ndani ya studio ya Free Nation ya Nay wa Mitego
Msanii wa muziki wa hip hop, Nay wa Mitego amemtambulisha producer mpya wa studio yake Free Nation Record baada ya kuachana na Mr T Touch.
Producer huyo akiwa ndani ya Free Nation Record
Rapper huyo ameonekana akiwa studio na producer huyo aitwae Osam wakirekodi wimbo mpya.
Producer huyo kupitia taarifa aliyoitoa kupitia Instagram, amedai amesainiwa studio hiyo ya Free Nation Record kama producer wa studio.
Nay wa Mitego na Mr T Touch wanadaiwa kuachana baada ya kushindwana kibiashara ambapo kwa sasa producer huyo amefungua studio mpya iliyopo Sinza Jijini Dar es salaam. Angalia picha za studio hiyo.
Nay wa Mitego akiandaa kazi mpya ndani ya studio hiyo