Picha: Jay-Z na Timbaland wapanda treni na kujichanganya na watu wa kawaida London
Jay Z amewapa ‘surprise’mashabiki wake wa nchini Uingereza baada ya kusafiri kwa treni jijini London kwenda kwenye show yake kwenye uwanja O2 Arena.
Akiwa kwenye treni, Jay Z aliungana na msanii wa kundi la Coldplay, Chris Martin na producer Timbaland, ambaye anamsaidia kwenye ziara yake ya dunia Magna Carta. Martin, ambaye ni rafiki mkubwa wa Jay Z, baadaye aliungana naye jukwaani.
http://www.youtube.com/watch?v=L4cU6c3FPhI
Shabiki aitwaye Jamie Robb alitweet picha baada ya kukutana na Jay kweny treni na kuandika, “What a riot… Just met Jay Z on the tube in London.”
Alieleza pia kuwa Jay Z alikuwa ameongoza na watu kama 10 hivi.
“Coming off the tube and I see Jay Z casually walking up the next escalator next to me… EVERYONE GOES NUTS,” alitweet shabiki mwingine.
Rihanna pia aliwahi kutumia usafiri huo alipokuwa na show nchini Uingereza.