Michezo

Picha: Juventus yatawala tuzo za Gran Gala del Calcio 2016/17

Usiku wa Jumatatu hii katika mji wa Milan zilifanyika sherehe za utoaji wa tuzo za Gran Gala del Calcio katika ligi kuu ya nchini Italia, timu ya Juventus ndio imeongoza kuzoa tuzo nyingi zaidi.

Timu hiyo imefanikiwa kushinda tuzo ya timu bora ya Italia baada ya kutwaa taji la ligi kuu ya nchi hiyo kwa mara sita mfululizo huku pia ikitoa wachezaji saba katika kikosi cha timu bora ya ligi ya Italia kwa mwaka 2016/17.

Wakati huo huo kocha wa Napoli, Maurizio Sarri amefanikiwa kushinda tuzo ya kocha bora na golikipa wa Juventus, Gianluigi Buffon amefanikiwa kunyakuwa tuzo mchezaji bora wa Serie A ambapo msimu uliopitta tuzo hiyo ilichukuliwa na Leonardo Bonucci.

Hii ndio timu bora ya Italia kwa msimu wa 2016/2017.

Gianluigi Buffon, Alex Sandro, Miralem Pjanic, Gonzalo Higuain na Paulo Dybala (wote kutoka Juventus), Dani Alves (PSG, msimu uliopita alikuwa Juventus), Leonardo Bonucci (AC Milan, msimu uliopita alikuwa Juventus).

Wachezaji wengine ambao wametajwa kwenye kikosi hiko ni pamoja na Kalidou Koulibaly, Marek Hamsik, Dries Mertens (Wote kutoka Napoli), na Radja Nainggolan (AS Roma).

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents