Promotion

Picha: Kampeni ya kutokomeza Malaria kwa kutumia simu za mkononi yazinduliwa jijini Dar

Malaria No More, ikishirikiana na Tanzania House of Talent na Vodacom Foundation Jumatano hii imefanya uzinduzi wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Malaria nchini kwa kutumia simu za mkononi. Uzinduzi huo umefanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Kampeni hiyo itaangalia jinsi teknolojia ya simu inavyoweza kutumiwa kiubunifu kuzungumzia masuala ya afya ya jamii kama Malaria.

Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alikuwa Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal pamoja na Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dkt Hussein Ali Mwinyi.

Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal akizungumza katika uzinduzi huo.
Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal akizungumza katika uzinduzi huo

Dkt Bilal alisema amependa kuona wasanii wa muziki wanatumia uwepo wao katika jamii kwa kufundisha na kuelimisha jamii katika mambo mbalimbali.

“Niwashukuru wasanii kwa kuendelea kupeleka ujumbe wakuelimisha kwa jamii, mnafanya kazi mzuri sana,na muziki unakuwa kwa kasi sana kuliko nchi nyingine,” alisema Dkt Bilal.

Pia Dkt Bilal alisema anawashukuru Vodacom kwa kuendelea kusaidia mambo muhimu nchini na pia kwa kuunda mfumo wa simu ambao utawawezesha Watanzania kupata taarifa za malaria. Aidha amewaomba Vodacom waendelee kusaidia ili taifa liendelee kukua.

Kwa upande wake Dkt Hussein Ali Mwinyi alisema serikali inatambua jitihada za mashirika mbalimbali katika kupambana na malaria nchini na kuongeza kuwa takwimu zinaonyesha jitihada za serikali zikishirikana na za mashirikika mbalimbali wameweza kupunguza vifo vya ugonjwa wa malaria.

Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza katika uzinduzi huo.
Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza katika uzinduzi huo

Picha ya pamoja wa viongozi pamoja na wadau waanzilishi wa kampeni ya kutokomeza malaria
Picha ya pamoja wa viongozi pamoja na wadau waanzilishi wa kampeni ya kutokomeza malaria

Katika kampeni hiyo, wananchi watakuwa na uwezo wa kutumia simu kufahamu taarifa mbalimbali kuhusiana na kujikinga na Malaria kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu, robo-calls na IVR (Interactive Voice Response). Ujumbe unaohusiana na Malaria utakuwa ukiwasilishwa na watu mashuhuri nchini akiwemo Rais Jakaya Kikwete.

Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa na Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal akiwa na Waziri wa afya na ustawi wa jamii Dkt. Hussein Ali Mwinyi

Akizungumza kwenye uzinduzi huo, mwakilishi kutoka THT, Ruge Mutahaba alisema wasanii watakuwa wakiimba nyimbo za kuhamasisha Watanzania njia mbalimbali za kujikinga na ugonjwa wa malaria kwakuwa wasanii hao wanap mashabiki wengi na kioo cha jamii hivyo kupitia wao ujumbe utafika kwa urahisi na kusaidia kutokomeza kwa kasi ugonjwa huo.
Mwakilishi kutoka THT Ruge Mtahaba akiongea katika uzinduzi huo.
Ruge Mutahaba akiongea katika uzinduzi huo

“Wasanii wanaweza wakawa mabalozi wakubwa sana katika kufikisha ujumbe wa kupambana na malaria kwa jamii hivyo tuliona tukiwatumia tutafanikiwa kutokemeza malaria kwa kiasi kikubwa sana,” alisema Ruge.

Vijana toka THT wakitoa burudani.
Vijana toka THT wakitoa burudani kwenye uzinduzi huo

Amini  na Barnaba  wakiimba kwa tabasamu.
Amini na Barnaba wakiimba kwa tabasamu

Barnaba akipeana mkono na Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal.
Msanii Barnaba akipeana mkono na Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal

Ben Pol akipeana mkono na Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal.
Ben Pol akipeana mkono na Makamu wa Rais Dkt Mohammed Gharib Bilal

Linah,Rachael,Barnaba na Amini wakitoa burudani.
Linah,Racho, Barnaba na Amini wakitoa burudani

Madee akiwa na Ben Pol.
Madee akiwa na Ben Pol

Madee na King Zilla.
Madee na King Zilla

Mkubwa na wanawe Babu Fela alikuwepo pia.
Babu Fela alikuwepo pia

Msanii wa muziki toka THT Asia akiwa na rafiki yake.
Kushoto msanii wa muziki toka THT Asia akiwa na rafiki yake

Mwakilishi kutoka No more Malaria Lilian akiongea katika uzinduzi huo.
Mwakilishi kutoka Malaria No More Lilian akiongea katika uzinduzi huo

Racheal
Racho

Ruge akiteta jambo na Makamo wa Rais  Dkt. Mohammed Gharib Bilal
Ruge akiteta jambo na Makamu wa Rais Dkt. Mohammed Gharib Bilal

Wadau ambao wamejitokeza kwa uzinduzi huo.
Wadau waliojitokeza kwenye uzinduzi huo

Wasanii toka THT
Wasanii toka THT

IMG_4619

IMG_4625

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents