Picha: Kifo cha Aaliyah chatimiza miaka 12 jana
Hollywood ilimpoteza staa wa R&B, Aaliyah miaka 12 iliyopita. Muimbaji huyo mzaliwa wa Brooklyn, alipoteza maisha kwenye ajali ya ndege Aug. 25, 2001. Alikuwa akitokea kwenye visiwa vya Bahamas, ambako alienda kushoot video ya wimbo wake “Rock The Boat”. Alikuwa na miaka 22 tu.
Aaliyah alianza kung’ara akiwa na umri mdogo. Alionekana kwenye show ya Star Search akiwa na miaka 10 na kisha kusainiwa na Jive Records miaka miwili baadaye.
Aaliyah na Damon Dash
R. Kelly alikuja kuwa mwalimu wake katika kipindi cha mwanzo cha career ya muziki ya Aaliyah. Alikuwa na vipaji vingi na kupitia muziki aliweza kutengeneza hits kibao “Are You That Somebody” na “Try Again.”
Aaliyah akiwa na Destiny’s Child
Pia alifanya vizuri kwenye filamu kwa kuigiza kwenye “Romeo Must Die” na “Queen of the Damned.”
Hadi sasa sauti yake bado inaendelea kutumiwa na wasanii wapya wakiwemo Drake na Chris Brown.
Atakumbukwa.