Michezo
Picha: Kobe Bryant aastafu kikapu kwa kufunga pointi 60
Kobe Bryant amecheza mchezo wake wa mwisho kwa nguvu ya ajabu kwa kuifungia timu yake, Los Angeles Lakers vikapu 60 alfajiri ya leo.
Mchezo huo dhidi ya Utah Jazz umemalizika kwa vikapu 101-96.
Ameutumia mchezo huo kuwaaga rasmi mashabiki wake baada ya kucheza kikapu kwa miaka 20. Mastaa mbalimbali wameendelea kumuaga kwenye mitandao ya kijamii.