Michezo
Picha: Lingard alivyosherehekea ushindi wa Man United na mpenzi wake wikiendi iliyopita
Mchezaji wa klabu ya Manchester United, Jesse Lingard amesherehekea ushindi wa mabao 2-0 walioupata timu yake dhidi ya Huddersfield, katika kombe la FA wikiendi hii na mpenzi wake ambaye ni mwanamitindo wa Marekani, Jena Frumes katika mgahawa wa Victor’s uliopo Hale nchini Uingereza.
Wawili hao ambao wamedumu kwenye mahusiano kwa takriban mwaka mmoja, wameonekana katika picha ya pamoja mitaani wakielekea katika mgahawa huo.