Picha: Magari ya kifahari ya mtoto wa rais wa Equatorial Guinea yenye thamani ya $4 mil. yapigwa mnada
Magari 11 ya kifahari yanayomilikiwa na mtoto ‘bitoz’ wa Rais Teodoro Obiang Nguema Mbasogo wa Equatorial Guinnea yenye thamani ya dola milioni 4.04 yamepigwa mnada jijini Paris, Ufaransa.
Magari hayo yalikamatwa na maafisa wa Ufaransa mwaka 2011 kutokana na madai kuwa yalinunuliwa kwa fedha za wizi za umma.
Magari hayo yaliyokamatwa ni pamoja na magari ya kifahari kabisa chini ya jua ambayo ni pamoja na Bugatti Veyrons mbili, Maserati MC12, Porsche Carrera GT, Ferrari Enzo na Ferrari 599 GTO.
Magari mengi kati ya hayo yalikuwa mapya na mengine hayajawahi kuendeshwa.
Dikteta huyo aliyekaa madarakani kwa miaka 30 anajulikana kwa maisha yake ya ‘kula bata’ ambapo alidaiwa kununua meli binafsi (yacht) yenye thamani ya dola milioni 380 mwaka 2011 na pia anamiliki nyumba yenye thamani ya dola milioni 35 huko Malibu, California nchini Marekani.