Michezo

Picha: Maji ya simamisha ujenzi uwanja wa Tottenham Hotspur

Ujenzi wa uwanja mpya wa klabu ya Tottenham Hotspur ulisimama kwa muda mwishoni mwa juma hili kufuatia kupasuka kwa ‘pipe’ kubwa iliyotiririsha maji kwa zaidi ya dakika 45 yaliyoelekea kwenye miundombinu ya umeme.

It reportedly took 45 minutes for the value to be closed

Mamia ya lita za maji yalimwagika siku ya Ijumaa na kufanya kusimama kwa ujenzi wa uwanja huo uliyogharimu mamilioni ya fedha wakati uzinduzi wake ukikusudiwa kufanyika mwezi Oktoba.

Water covers electrical equipment and wires in the new stadium

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 8.45 asubuhi siku ya Ijumaa na kupelekea wafanyakazi kuhaha katika kuhakikisha wanazuia tatizo hilo.

The builders behind the new stadium recently revealed faulty wiring is behind the delay

Chanzo kimoja cha habari kimesema kuwa maji mengi yalimwagika baada ya ‘pipe’ kubwa ya maji kupasuka wakati watu wakiwa wanafanyakazi.

Tottenham still hope to host their first game at the stadium against Man City on October 28

Na kusisitiza kuwa mabosi wote wanaowasimamia wafanyakazi walilazimika kushuka chini sehemu ya kiwanja ili kuhakikisha wanalizuia tatizo hilo huku maji hayo yakionekana kusambaa kwenye miundombinu ya umeme.

Mapema mwezi huu, Spurs ilitangaza kuwa mpaka mwezi wa Oktoba Tottenham Hotspur itahamia kwenye uwanja wake mpya.

Related Articles

2 Comments

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents