Habari

Picha: Makonda aanza kuhojiwa na bunge Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Jumanne hii ameanza kuhojiwa na Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kujibu tuhuma zinazomkabili za kuingilia Haki, Uhuru na Madaraka ya Bunge.

Kwa mujibu wa maelezo kwenye akaunti maalum ya Facebook ya bunge hilo, wito wa kufika mbele ya kamati hiyo umefikiwa kufuatia azimio la Bunge kumuomba Mhe Spika kuwaita mbele ya kamati wakuu wa wilaya na mikoa waliotoa matamshi ya kudharau mamlaka ya Bunge.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents