Michezo
Picha: Mamadou Sakho na familia yake wanavyozidi kuipa shavu Tanzania
Mamadou Sakho anayechezea klabu ya soka ya Liverpool ya Uingereza ambaye yupo nchini na familia yake kwa ajili ya mapumziko wameonyesha kuyafurahia mazingira ya Tanzania kutokana na vivutio vilivyopo.
Mke wa mchezaji huo Majda Sakho amethibitisha hilo kwa kuweka picha tatu katika mtandao wa Instagram zikiwaonyesha wakiwa katika mbuga ya wanyama ya Serengeti iliyopo mkoani Manyara pamoja na watoto wao Aïda na Sienna.
“?Another family day in Tanzania ? #family #familyfirst #vacations #love #blessed #africa #summer17 #instamoments #instalikes #instafamily #instadaily @mamadousakho3,” ameandika kwenye picha hiyo hapo juu aliyoiweka katika mtandao huo.