Michezo
Picha: Man United warudi kinyonge Uingereza baada ya kipigo cha Bayern Munich
Kikosi cha Manchester United kimerejea nchini Uingereza asubuhi ya leo mara baada ya kumaliza ziara yao ya kujiandaa na msimu mpya wa ligi.
United ilikubali kipigo cha bao 1 – 0 dhidi ya Bayern Munich hapo jana usiku wakati Javi Martinez akitupia goli hilo ambalo liliwatofautisha na mashetani wekundu.
Sasa Man United inajipanga na michezo mbalimbali ya ligi kuu Uingereza inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.
Mourinho anatarajia kukabiliana na Leicester kwenye mchezo wake wa kwanza siku ya Ijumaa majira ya usiku.
Haha