Picha: Mapacha, Mkoloni, Profesa Jay, Abby Sykes na Black Rhyno wakibariki Kilinge cha March 2
Kilinge cha Tamaduni Muzik ambacho hufanyika kila siku za Jumamosi pale Msasani Club jijini Dar es Salaam kilianza kama utani lakini sasa hivi kimekua na mastaa kibao wa Hip Hop ya Tanzania wameanza kujitokeza na kuperform.
Ni sehemu ambapo wasanii wa hip hop wanaimba kwa passion na si kwaajili ya fedha. Ni sehemu ambapo wanajibrush uwezo wao kwenye stage mbele ya mamc wengine wakali. It’s about having fun and showing the love for Hip Hop.
Kinachofurahisha zaidi ni wahudhuriaji wa Kilinge hicho ambao hakika ni mashabiki wa Hip Hop damu damu. Jana Profesa Jay alihudhuria kwa mara ya pili na hii ni baada ya kuona umuhimu wa kuhudhuria huku Mapacha, Mkoloni, Mzee Abby Sykes (baba yake na Dully Sykes) na Black Rhyno nao wakishika kipaza kuonesha uwezo wao wakisindikizwa na mamc waanzilishi wa Kilinge hicho kutoka Tamaduni Muzik.
Hizi ni picha za kilinge cha March 2, 2013. Picha na Ngome Video Facebook