Picha: Mashindano ya foosball yazinduliwa kwa mara nyingine jijini Dar
Kampuni ya bia ya Heineken jana katika hotel ya Kempiski jijini Dar es salaam imezindua msimu wa pili wa kampeni ya michuano ya Foosball kwa nchi za Afrika Mashariki ambapo itaanza kufanyika hivi karibuni kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini.
Mkurugenzi mkuu wa Heineken Tanzania, Uche Unigwe akiwa na washindi wa foosball mwaka 2013
Akizungumza katika uzinduzi huo ,Mkurugenzi mkuu wa Heineken Tanzania Uche Unigwe alisema kuwa wameamua kuzindua mchezo huo baada ya mashabiki kuhamasika zaidi.
“Foosball ambayo inachezwa na mashabiki wengi ulimwenguni,umekua kati ya michezo inayokuwa zaidi kila siku na hivyo tumeamua kuzindua tena kampeni hii ili kuendelea kuongeza mashabiki wa soka. Kwa mwaka wa pili mfululizo Heineken inaendesha michuano ya foosball,baada ya kufanya vizuri msimu uliyopita,hivyo tunatarajia mashabiki wa soka wataongeza ufanisi zaidi kwenye msimu huu,” alisema Uche
Mkurugenzi mkuu wa Heineken Tanzania Uche Unigwe akiwa na wamiliki wa bar ambazo zitachezeka mchezo wa foosball mwaka huu
Mkurugenzi mkuu wa Heineken Tanzania Uche Unigwe akizungumza na Kibonde
Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania Uche Unigwe