Habari
Picha: Matukio ya shambulio la Westgate yageuka mtaji Nairobi, movie za tukio hilo zaanza kuuzwa mitaani
Ikiwa ni zaidi ya wiki moja toka shambulio la kigaidi litikise jiji la Nairobi, Kenya katika jengo la biashara Westgate, tayari wafanyabiashara wa Kenya wameanza kutumia tukio hilo lililochukua maisha ya watu na kuleta hasara kubwa, kujinufaisha kutokana na tukio hilo.
Video za tukio hilo sasa zimekusanywa na kuwekwa katika DVD na kuuzwa mitaani na wafanyabiashara wa jiji la Nairobi.
Kwa mujibu wa Nairobi Wire movie hizo za Westgate zinapatikana kwa majina tofauti na covers tofauti na zimeonekana kufanya vizuri japokuwa kilichomo ndani ni mkusanyiko wa habari tu za matukio mbalimbali ya shambulio hilo la kigaidi katika video.
Picha: Nairobi Wire