Habari
Picha: Mazishi ya Mama Lucy Kibaki yalivyofanyika huko Kenya
Siku ya Jumamosi yalifanyika mazishi ya mke wa rais mstaafu wa Kenya, Mama Lucy Kibaki.
Mazishi hayo ya Mama Lucy yalifanyika kwenye makaburi ya Kibaki’s Kanyange ambako viongozi kadhaa walihudhuria mazishi hayo akiwemo rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta na rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
Hata hivyo wakati wa mazishi vyombo vya habari havikuruhusiwa kufika kwenye maeneo ya makaburi.
Mama Lucy Kibaki Kibaki alifariki siku ya Jumanne, April 26 kwenye hospitali ya Bupa Cromwell iliyopo jijini London, nchini Uingereza.
Hizi ni baadhi ya picha za mazishi ya Mama Lucy Kibaki.