Habari
Picha: Mazishi ya mtangazaji wa EFM yalivyofanyika kwenye makaburi ya Kinondoni
Hatimaye Seth Katende maarufu kama Bikira wa Kisukuma ambaye alikuwa mtangazaji wa kipindi cha Ubaoni cha EFM, amezikwa mchana huu katika makaburi ya Kinondoni baada ya taratibu za kuuwaga mwili wa marehemu kukamilika katika viwanja vya Leaders Club.
Katika mazishi hayo yam,ehudhuriwa na umati mkubwa wa watu, wakiwemo wasanii, watangazaji kutoka vituo mbalimbali, viongozi wa serikali, wanasiasa na watu wengine maarufu. Hizi ni baadhi ya picha wakati wa mazishi hayo.
Picha ya mtoto wa marehemu akiwa amebebwa