Picha

Picha: Mchezaji mstaafu wa timu ya football ya Marekani, Ravens, Ray Lewis ashindwa kupanda Mt. Kilimanjaro baada ya kupata homa

Mchezaji mstaafu wa timu ya football ya Marekani, Baltimore Ravens, Ray Lewis wiki iliyopita alishindwa kuupanda Mlima Kilimanjaro kutokana kuumia mguu na kupata homa.

b74e4af7a9fa1187a8a25b01913c0ece_large

Lewis alikuja kuzitembelea nchini za Afrika Mashariki na juzi alikuwa Dar es Salaam ambapo pia alikutana na Rais Jakaya Kikwete aliyempa zawadi ya kofia ya timu ya Ravens.

c96418e0d462e96e3e6b8888e7c6b433_large
Lewis alitumia muda wa saa nzima kuzungumza na Rais Kikwete ambaye alimwalika kuja tena Tanzania siku za usoni.

Mchezaji huyo yupo Afrika Mashariki kwenye mradi wa kusaidia upatikanaji wa maji safi na salama na ameongoza na mchezaji wa zamani wa Chicago Bears Pro Bowl, Tommie Harris na Doug Pitt, kaka yake na muigizaji Brad Pitt ambaye ni balozi mwema wa Tanzania.

1a4b8e4bd33157c183dc677ac27c9d61_large

Bila Lewis, kundi hilo lilifanikiwa kuupanda mlima huo mrefu zaidi barani Afrika wenye futi 19,340. Lewis na kundi lake walitoa msaada wa vifaa vya kusaidia watu wenye ulemavu wa kusikia na pia alitembelea kituo cha kulelea watoto yatima.

bed7222573eda183bbab5af585052e1e_large

Ray akizungumza na mtoto
Ray akizungumza na mtoto

Ray na watoto
Ray na watoto

Ray akiwaonesha kitu watoto
Ray akiwaonesha kitu watoto huko Moshi, Kilimanjaro

acb5d5349856a48e6f8efa8126e23a0b_large

fb64e6b02cf1c6863f043817d4b53924_large

Pia mchezaji huyo alitumia muda wake na watoto hao ambao aliwaomba waandike mahitaji yao kwenye karatasi.

9f0368af392e3ef4f80889854ac7e530_large

a1835d0531c263145905c04253ba9031_large

Kabla ya kuondoka, Lewis aliweka alama ya mkono kwenye ukuta wa darasa.

f7353ec6b365ac6b8a6c4255bc4345eb_large

Baada ya kuona kuwa hawezi kupanda mlima Kilimanjaro kutokana na hali yake ya kiafya, Lewis alizungumza kwenye video kuhusu msaada wake kwa Afrika.

“Kitu kikubwa tulichonacho kwenye maisha ni fursa,” anasema Lewis. “Ni kwa kufanya kupitia fursa ndio kunaweza kuacha urithi usioisha. Timu hii tuliiweka kwenda kubadilisha maisha na maisha na kuwashika watu ambao hawatajua hata majina yetu lakini watakumbuka urithi wetu kutokana na kile tulichokifanya kuleta maji safi kwenye ardhi ya mama zetu kwa watu wasiojiweza na kuwapa fursa ya pili.”

Lewis, 38, aliyestaafu baada ya kushinda Super Bowl ya pili akiwa na Ravens, kwa sasa anafanya kazi na kituo cha ESPN kama mchambuzi wa football. Aliongozana na mashirika ya WorldServe International na TackleKili kwenye ziara hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents