Habari
Picha: Bosi wa Kaburu Entertainment atumia birthday yake kumtambulisha Amber Lulu kuwa ni mpenzi wake
Mkurugenzi wa label ya Kaburu Entertainment, Mr Kaburu weekend hii alifanya sherehe ya birthday yake ambayo iliambatana na kumtambulisha mpenzi wake ‘Amber Lulu’.
Kaburu akiwa na Amber Lulu
Shughuli hiyo iliyohudhuriwa na mastaa mbalimbali wa muziki nchini, ilifanyika nyumbani kwake huko Bunju B jijini Dar es salaam.
Akiongea na ndugu jamaa na marafiki muda mchache baada ya kumaliza shughuli hiyo, alisema ameamua kumtambulisha Amber Lulu kwa jamii ili kieleweke kinachoendela kati yao.
Alisema walikuwa kimya kwa muda mrefu kuhusu mahusiano na mrembo huyo kwa kuwa hawakuhafikiana kuweka wazi juu ya mahusiano yao.
Producer wa Kaburu Record
Meneja wa Mr Ttouch, Sudy Baya (kushoto) akiwa na producer wa Kaburu Record