Michezo
Picha: Muonekano mpya wa bingwa wa WWE, John Cena washtua mashabiki
Mcheza mieleka maarufu duniani, John Cena amewashangaza mashabiki zake wanaofuatilia WWE baada ya kuposti muonekano wake mpya kupitia mitandao yake ya kijamii akiwa Shanghai kwenye maandalizi ya filamu ya Jackie Chan.
Bingwa huyo wa Dunia mara 16 hajaingia ulingoni kupambana kwa muda mrefu tangu afanye hivyo mwezi Aprili nchini Saudi Arabia dhidi ya Triple H.
Hata hivyo mbabe huyo mwenye umri wa miaka 41 ameonekana mwili wake kuimarika zaidi ukilinganisha na hapo awali huku akitarajiwa kuonekana kwenye filamu mpya ya Jackie Chan inayotarajiwa kutoka mwakani 2019 akichukua nafasi ya Sylvester Stallone kwenye move hiyo inayokwenda kwa jina la ‘Project x’ .
Mbona kama anapiga chafya…
Matumizi ya vidonge ambayo hata bongo Siku hizi wanatumia sana wabeba vitu vizito
Duh!!???
Hatarii
Kwani John Cena si nikisikia amekufa jamaani au uzushi 😢😢😢😢😢