Habari

Picha: Mwili wa Ivan Ssemwanga ulivyowasili Uganda

Hatimaye mwili wa tajiri Ivan Ssemwanga aliyefariki wiki iliyopita nchini Afrika Kusini kutokana na ugonjwa wa moyo umewasili Jumapili hii nchini Uganda kwa ajili ya kufanyiwa mazishi.

Mwili hu uliwasili majira ya mchana katika gari aina ya A-Plus Mercedes-Benz wakitokea katika uwanja wa ndege huku magari mengi ya kifahari yakiongozana na msafara huo.

Zari ambaye alizaa na marehemu watoto watatu akiwemo Quincy, Raphael na Pinto aliongozana na wanae hao katika msafara huo. Ivan anatarajiwa kuzikwa kesho (Jumanne). Hizi ni baadhi ya picha za tukio hilo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents