Picha
Picha: Nas na mwanzilishi wa Facebook Mark Zuckerberg waongea biashara!!
Rapper Nas weekend hii alijumuika kwenye chakula cha usiku na miongoni mwa madon kwenye biashara ya technolojia, CEO wa Facebook Mark Zuckerberg (na mke wake Priscilla) pamoja na bilionea Ben Horowitz.
Kama ukipata muda wa kula chakula na mabilionea, ni wazi kuwa maongezi yalihusu pesa na uwekezaji.Picha za watatu hao zilizoenea kwenye mtandao wa Instagram zimezua maswali mengi lakini wengi wanahisi Nas anaweza kupewa mchongo wa maana na Facebook, ambayo inamilikiwa na Mark na Ben akiwa amewekeza kupitia kampuni yake tajiri ya Andreessen Horowitz.