Technology

Picha: NASA yatoa picha ya kwanza ya sayari ya Jupiter iliyotumwa na Juno

Chombo cha anga za juu cha shirika la Marekani la NASA kilichopewa jina Juno kimetuma picha za kwanza za sayari ya Jupiter.
13juno-superJumbo
Picha ya kwanza iliyotumwa na Juno

Picha hiyo iliyotolewa na NASA Jumanne hii inaonesha sayari hiyo ikiwa imezungukwa na miezi mitatu kati ya miezi yake minne mikubwa.

Miezi inayoonekana ni Lo, Europa na Ganymede. Mwezi huo mwingine uitwao Callisto hauonekani.
A model o, map the magnetic field, and measure the amount of water and ammonia in the atmosphere. Photo Credit: (NASA/Aubrey Gemignani)

Picha hiyo ilipigwa Jumamosi wakati Juno ilipokuwa inazunguka sayari hiyo ikiwa umbali wa maili milioni tatu.

Hata katika umbali huo, Shimo Jekundu, lililosababishwa na dhoruba kali kwenye sayari hiyo karne nyingi zilizopita, linaonekana.

Juno iliingia katika mzingo wa Jupiter wiki iliyopita na kuanza kuizunguka sayari hiyo ambalo pia hufahamika kama Zohali au Zozali.

Safari yake kutoka duniani hadi ilichukua miaka mitano.

Juno itachunguza na kupeleleza sayari hiyo kwa miezi 20, lengo kuu likiwa kusaidia wanasayansi kubaini asili ya sayari hiyo ambayo wanaamini inaweza kuwasaidia kuelewa zaidi asili ya mfumo wa jua.

Chombo hicho cha juu kilipokuwa kinaikaribia Jupiter, kamera zake na mitambo mingine muhimu vilizimwa kuzuia visiharibiwe na miali nururishi. Baadaye, vilifunguliwa.

Wanasayansi wanatarajia picha za karibu zaidi za Jupiter zitapokelewa mwezi ujao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents