Habari
Picha: Ndoa yanukia kwa Size 8 wa Kenya!
Linet Munyali maarufu zaidi kwa jina la Size 8 alitokea katika vichwa vingi vya habari mwanzoni mwa mwaka huu baada ya kuwasurprise watu kwa kuamua kubadili njia yake ya kiimani kwa kuokoka na kuanza kufanya muziki wa gospel.
Ijumaa (July 5) Size 8 kutoka Kenya amewasurprise tena mashabiki wake baada ya kutweet picha ya vazi jeupe ambalo hutumika katika shughuli muhimu na maalum katika maisha ya mwanadamu (ndoa) na kuisindikiza na maneno mawili mafupi yanayoashiria anategemea kuolewa hivi karibuni.
Very soon!!!! pic.twitter.com/tXQ2I5z2HP
— Size8 (@size8reborn) July 5, 2013
Juu ya picha hiyo Size 8 aliandika “Very soon!!!!”
Bila shaka hivi karibuni tutafahamu who is the lucky guy!