Burudani

Picha: Nyumba aliyokuwa akiishi Madonna yaingizwa sokoni kwa $479k

Nyumba aliyokuwa akiishi malkia wa muziki wa pop duniani Madonna katika kipindi cha utoto wake akiwa pamoja na wazazi wake imeingizwa sokoni.

Nyumba hiyo ambayo ipo katika mji wa Detroit katika jimbo la Michigan nchini Marekani, iliungua kwa moto mwaka 2008 na iliachwa wazi mpaka kufikia mwaka 2012 ndipo ilipouzwa kwa kiasi cha shilingi milioni 205,041,035 kwa fedha za kitanzania.

Lakini kwa sasa nyumba hiyo yenye vyumba vitano vya kulala, mabafu matatu, ambayo ilitengenezwa vizuri na mwenye nyumba huyo mpya inauzwa kwa kiasi cha dola 479,900 ambapo kwa fedha za kibongo ni sawa na shilingi 1,073,226,252.

Hizi ni baadhi ya picha za nyumba hiyo.

Kwa sasa nymba hiyo kubwa iliyona vyumba vya kulala vitanao na mabafu mawili ya kuogea inauzwa kwa dola za kimarekani 479,900 sawa na shilingi bilioni moja na zaidi, mnana wa nyumba hiyo utafanywa siku ya jumamaposi kuanzia saa 11 jioni hadi saa mbili usiku.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents