Burudani

Picha: Ommy Dimpoz akutana na balozi wa Tanzania nchini Marekani Liberata Mulamula

Omar Nyembo aka Ommy Dimpoz, jana alipata fursa ya kukutana na balozi wa Tanzania nchini Marekani, Bi. Lebarata Mulamula kwenye ubalozi wake uliopo mjini Washington DC, Marekani.

IMG-20131003-WA001
Ommy Dimpoz akiwa na balozi Mulamula ambaye amekuwa balozi wa pili wa kike kuiwakilisha Tanzania nchini Marekani, baada ya Mwanaidi Maajar

IMG-20131003-WA000
Ommy Dimpoz, Balozi Mulamula na maafisa wengine katika ubalozi wa Tanzania nchini Marekani

“Niliongea naye mambo mengi kuhusu muziki wa Bongo Flava na vijana tunavyotumia fursa na vipaji vyetu kujiajiri,” Ommy ameiambia Bongo5.

IMG-20131003-WA003
Ommy Dimpoz akiangalia picha za waliowahi kuwa mabalozi wa Tanzania nchini Marekani

IMG-20131003-WA002
Ommy akiwa na Bi. Mulamula ambaye kabla ya uteuzi huo, aliwahi kuwa Msaidizi Mwandamizi wa Rais katika masuala ya kidiplomasia na aliwahi kuwa Katibu Mtendaji wa Kwanza kuiongoza Sekretarieti ya Nchi za Maziwa Makuu kwa kipindi cha miaka minne kuanzia Januari, 2007 hadi Desemba, 2010
IMG-20131003-WA004
Ommy Dimpoz akisaini kitabu cha wageni kwenye ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
IMG-20131003-WA005
Ommy Dimpoz akiwa kwenye mazungumzo na Balozi Mulamula pamoja na maafisa wengine wa ubalozi huo

IMG-20131003-WA011
Ommy, Bi. Mulamula na Mkurugenzi wa MMK Media Group LLC , Dickson Mkama aka DMK

Wakati huo huo, Ommy aliyeenda nchini humo kwa ziara ya wiki tatu, amerekodi wimbo kwenye studio ya Xtrem Recs ya Houston, Texas ambapo producer ni Giggz kutoka Kenya.

IMG-20131003-WA008
Ommy akiwa kwenye studio za Xtrem Recs

IMG-20131003-WA009
Giggs ambaye Ommy amesema amefanya kazi na wasanii wakubwa kama Davido, Wizkid na Tuface

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents