Picha
Picha: P-Square wakisimamia ujenzi wa jumba lao jipya, Nigeria
Inaonekana jumba la SquareVille la mapacha wanaopendwa zaidi Afrika, P-Square haliwatoshi na ndio maana wameamua kupandisha mansion nyingine.
Ndugu hao wa Okoyes wanadaiwa kuwa na ujenzi wa jumba jingine la kifahari huko ParkView Estate maeneo ya Ikoyi, Lagos. Ujenzi wa nyumba jumba hilo ulianza mwaka jana wakati wasanii hao walipokuwa na ziara katika nchi za Afrika.
Hizi ni picha zilizowekwa na Jude Okoye kwenye page ya Instagram zikimuonesha akiwa na mdogo wake Peter Okoye kutazama maendeleo ya ujenzi huo.
January 2013, ndugu hao walinunua jumba jingine jijini San Francisco, Marekani. Mapacha hao juzi walikuwa na show nchini Angola na kujaza nyomi ya kufa mtu.