Bongo Movie

Picha: Pambano dhidi ya Bongo Movies na Bongo Fleva

Mamia kwa maelfu ya wakazi wa jiji la Dar-Es-Salaam na vitongoji vyake walifurika katika uwanja mkuu wa taifa kushuhudia tamasha la burudani mbali mbali za kimuziki, Ndondi pamoja na mpira wa miguu uliohusisha wabunge wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania wanaoshabikia timu za Yanga na Simba, Bongo Flava dhidi ya Bongo Muvi, mpambano wa Wema na Jackline Wolper na mwisho kabisa Ngumi kati ya bondia Japhet Kaseba na Francis Cheka.
Tamasha hilo lililoandaliwa kwa pamoja baina ya Kampuni ya Global Publishers kupitia kitengo chake cha Burudani kwa kutumia platform yao ya ukumbi wa burudani Dar Live, pamoja na mfuko wa elimu na kulipa jina tukio hilo kuwa la Tamasha La Matumaini lilikuwa mahususi kuchangia mfuko wa elimu kwa wasichana katika ujenzi wa mabweni katika shule ya Kongwa mkoani Dodoma…
Watu wa marika mbali mbali walihudhuria tamasha hilo ambalo lilianza rasmi majira ya saa tisa kamili ambapo timu ya Bongo Fleva ilipambana na timu ya Bongo Muvi na timu ya Bongo Fleva kuondoka na ushindi wa goli moja dhidi ya Bongo Fleva katika pambano lililokuwa la kuvutia na vituko pamoja na vibweka kibao. Alikuwa… ambaye aliwainua mashabiki wa Bongo Muvi baada ya kufunga goli katika dakika ya 64 ya kipindi cha pili.
Mastaa kama Claude 112, Steve Nyerere, Abdul Kiba, H baba, TID, Inspector Harun, Vincent Ray kigosi na wengineo walitoa burudani ya kutosha kwa kucheza mpira uliofurahisha na kusisimua wengi. Aidha burudani kubwa ilikuwa baada ya kipyenga cha refa Othman kazi kupulizwa kuashiria mechi imeisha ambapo wachezaji wa Bongo muvi walikwenda kushangilia ushindi kwa mashabiki wao huku wakicheza kwaito na steve Nyerere kuvua jezi yake na kuonyesha maandishi ya “why Always Me? ”. kitendo kilichofanya wamfananishe na Balotelli

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents