Picha: Poetry Addiction 3rd FIX – Triniti Dar es Salaam
Kampuni ya Cheusi Dawa ya Fid Q, jana ilifanikisha kwa mara ya tatu kuandaa showya Poetry Addiction aka ‘Uraibu wa Ushairi’ iliyofanyika kwenye ukumbi wa Triniti jijini Dar es Salaam. Show ya jana ilishuhudia wasichana pekee wakitumbuiza wakiwemo, Aichi, Kethi, Charlotte O’Neal maarufu kama Mama C, Jade, Vanessa Mdee, Grace Matata, Elizabeth Mwakijambile na wengine.
Aichi akiliweka sawa gitaa lake tayari kuanza kutoa burudani
Hii ni mara ya tatu Fid Q ameandaa Poetry Addiction akishirikiana na Choice FM ambayo hufanyika kila mwezi
Grace Matata akiimba kwa hisia
Charlotte O’Neal aka Mama C akitumbuiza
One the Incredible akiwa na Grace Matata wakibadilishana mawili matatu
Watu walijitokeza kwa wingi ikiwa ni ishara kuwa Poetry Addition inaendelea kukua zaidi
Elizabeth Mwakijambile, Epiq Bongo Star Search (kushoto) akitumbuiza
Watu wa kila aina walijitokeza jana kushuhudia burudani ya live band
Mwanadada Aichi akionesha ujuzi wa kuimba huku akicharaza gitaa
Watazamaji wakifurahia tumbuizo la ‘Uraibu wa Ushairi’
Aichi (kushoto) akifurahia jambo
Profesa Ludigo (katikati) akiteta kitu na rafiki yake