Siasa
Picha: Rais Jakaya Kikwete aongoza mazishi ya Bi. Kidude
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, leo ameongoza mazishi ya mwanamuziki mkongwe wa Taarab nchini, Fatuma binti Baraka maarufu kama Bi. Kidude.
Bi Kidude alifariki dunia jana kutokana na kusumbuliwa na maradhi ya sukari na uvimbe kwenye kongosho. Mazishi hayo yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, watu mashuhuri, wasanii na watu wengine mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi. Hizi ni picha za mazishi hayo.