Siasa
Picha: Rais Kikwete aongoza Watanzania kwenye mazishi ya Sajuki
Mamia ya wapenzi wadau, ndugu jamaa na marafiki wakiongozwa na mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Kikwete pamoja na baba mzazi wa Sajuki leo mchana wamehudhuria maziko ya msanii wa Filamu Juma Kilowoko (Sajuki) katika makaburi ya Kisutu Upanga jijini Dar-Es-Salaam.
Msanii huyo alifariki asubuhi ya jumatano ya tarehe 2 katika hospitali ya taifa ya Muhimbili baada ya kuugua kwa muda mrefu kiasi. Katika safari yake hiyo ya mwisho Sajuki aliagwa na mamia ya wakazi wa jijini Dar-Es-Salaam akiwemo Meya wa Ilala Jerry Slaa, Mbunge wa Kinondoni Iddi Azzan, Zitto Kabwe, wana filamu wenzake na wadau mbali mbali.
Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu Sajuki. Amen