Habari
Picha: Rais Magufuli alivyomuapisha Naibu Waziri Wizara ya Madini leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo Jumatatu amemnuapisha Naibu Waziri wa Madini, Mh. Doto Mashaka Biteko ikulu jijini Dar es Salaam.
Mh. Doto ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe na pia alikuwa Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite aliteuliwa katika nafasi hiyo Jumamosi ya January 6 mwaka huu ambapo katika wizara hiyo kwa sasa itakuwa na Waziri pamoja na Manaibu Waziri wawili.