Habari
Picha: Rais Magufuli amjulia hali Mzee Kingunge
Rais Dkt. John Magufuli amemjulia hali Mzee Kingunge Ngombale Mwiru aliyelazwa katika wodi ya Mwaisela, Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Mzee Kingunge anatibiwa majeraha baada ya kushambuliwa na mbwa nyumbani kwake. Hali ya mzee Kingunge inaendelea vizuri kwa sasa.