Burudani
Picha: Saa hii ya Davido ina thamani ya shilingi milioni 264
Saa mpya anayovaa Davido inaweza kujenga nyumba ya kifahari.
Saa hiyo aina ya Rolex Oyster Perpetual Datejust inauzwa $120,000 ambazo ni takriban shilingi milioni 264 za Tanzania.
Staa huyo aliamua kutumia snapchat kuitaja bei ya saa hiyo baada ya watu wengi kutaka kujua gharama yake.
Staa huyo wa Nigeria aliyesainishwa na label ya Sony hivi karibuni anafahamika kwa maisha yake ya kifahari na anamiliki pia mjengo huko Atlanta, Marekani.