Habari
Picha: Trump na mkewe Melania walivyowatembelea majeruhi waliopigwa risasi Florida
Rais wa Marekani Donald Trump na mkewe Melania wamewatembelea hospitalini wanafunzi ambao wamejeuhiwa kwa kupigwa na risasi kwenye shambulio lilofanywa katika shule ya Parkland mjini Florida siku ya Jumatano.
Tukio hilo ambalo lilifanywa na mwanafunzi wa shule hiyo mwenye miaka 19, Nikolaus Cruz lilisababisha vifo vya watu 17 na wengine 15 kujeruhiwa.
Ilidaiwa kuwa Cruz alitekeleza shambulio hilo kutokana na madai ya kufukuzwa shule kutokana na utovu wa nidhamu. Hata hivyo polisi walifanikiwa kumkamata kijana huyo.