Picha
Picha: Uzinduzi wa Redd’s Miss Tanzania 2013
Shindano la Redd’s Miss Tanzania 2013 jana limezinduliwa rasmi katika hoteli ya Serena na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.
Uzinduzi huo uliandaliwa na wadhamini wakuu wa shindano hilo, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji cha Redd’s ambao uliwakutanisha wapenzi wa urembo na wadau mbalimbali, wakiwemo mawakala wanaoandaa mashindano ya kumsaka Redd’s Miss Tanzania katika hatua za awali, kanda, mikoa hadi taifa.
Katika uzinduzi huo Redd’s Miss Tanzania, Brigite Alfred alikuwepo sambamba na Miss Tanzania wa zamani wakiwemo Nancy Sumari, Faraja Kotta na Salha Israel.
Uzinduzi huo unamaanisha kuwa mawakala wote wataanza mchakato wa kuandaa mashindano katika ngazi za wilaya, mikoa, kanda na baadaye taifa.