Technology
Picha, Video na vingine havihesabiki tena kwenye maneno 140 ya Twitter
Twitter imeamua kuwapa zawadi watumiaji wake. Kuanza sasa, viambatanisho kama vile picha, video au kunukuu tweet nyingine, havitahesabika kwenye maneno 140.
Kampuni hiyo imetangaza hatua hiyo Jumatatu hii.
Miaka ya hivi karibuni, Twitter imekuwa ikitapatapata kwendana na ushindani wa mitandao ya kijamii. Tayari ipo nyuma ya Facebook, Instagram na Snapchat kwa nyuma kwa umaarufu.
Bado imekwama pale pale na watumiaji milioni 300 na tangu iende public November 2013 haijaanza kupata faida. Tatizo kubwa la Twitter ni kushindwa kupata watumiaji wapya wanaoweza kuifurahia.