Habari

Picha: Wananchi wa Romania waendelea kuandamana kupinga sheria ya rushwa

Maelfu ya watu wamekusanyika katika maeneo mbalimbali ya jiji la Bucharest pamoja na miji mingine ya nchini Romania kuanzia usiku wa Jumatano hii kupinga sheria ya kuhalalisha baadhi ya matendo ya rushwa iliyopitishwa na serikali ya nchi hiyo.

Kupitia sheria hiyo imewakingia kifua viongozi wa nchi hiyo wasiokuwa waaminifu kutopelekwa mahakamani iwapo kesi zao zitahusisha ufujaji wa fedha chini ya dola 48,000. Hayo yalikuwa ni maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea kwenye nchi hiyo yenye raia zaidi ya milioni 19.96 tangu Disemba 1989 ulipoanguka utawala wa kikomunisti katika nchi hiyo.

Tazama picha za maandamano hayo hapa chini.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents