Habari

Picha: Watu 14 wajeruhiwa mjini Melbourne, Australia

Watu zaidi ya 14 wamejeruhiwa kwa kugongwa na gari lililokuwa likiendeshwa kwa mwendo kasi katika mji wa Melbourne nchini Australia.

Ajali hiyo iliyotokea imetajwa kutokea katika makutano ya barabara za mtaa wa Elizabeth na Flinders mjini humo mapema leo ambapo miongoni mwa watu waliojeruhiwa ni mtoto mdogo ambaye hali yake siyo nzuri.

Hata hivyo polisi wamefanikiwa kuwakamata watu wawili ambao walikuwepo katika gari lililosababisha ajali hiyo akiwemo dereva aliyekuwa anaendesha.

Polisi wamesema inaamini kitendo hicho kimefanywa kwa kukusudia lakini bado wanaendelea na uchunguzi.


Picha ya dereva wa gari lililosababisha ajali akiwa amekamatwa na polisi

Pedestrians walk past as police and emergency services attend the scene of an incident involving a vehicle and pedestrians in Melbourne, Thursday, Dec. 21, 2017. Police have arrested a driver after a car drove into pedestrians on a sidewalk in central Melbourne. (Kaitlyn Offer/AAP Image via AP)


Picha ya mtu mwengine aliyekuwepo katika gari lililosababisha ajali akichukuliwa maelezo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents