Jana Miss Tanzania wa zamani na muigizaji wa filamu nchini, Wema Sepetu alifanya uzinduzi wa ofisi za kampuni yake ya Endless Fame Films jijini Dar es Salaam.
Katika uzinduzi huo, mrembo huyo aliwaalika waandishi wa habari na pia uzinduzi huo kuhudhuriwa na waigizaji wenzie akiwemo JB, Richie Richie, Ray, Dotnata na wengine.
Akizungumzia sababu za kuanzisha kampuni hiyo, Wema alisema, “lengo kubwa kabisa ni kuempower young talents, kupromote vipaji vipya na kufanya kazi at a more advanced level and most importantly ni kuimprove quality za kazi za kitanzania.”
Alisema kazi rasmi za kampuni yake zitaanza mwezi ujao na tayari ameshaajiri wafanyakazi ingawa bado anakaribisha maombi yake kazi.
“Ukijua kwamba una kipaji na you have a reason to work with Wema Sepetu then why not, bring your application ntago through it if your CV works then…….”
Akizungumzia filamu yake ya Supastaa, Wema amesema ilikuwa imeshaanza kueditiwa na sasa ipo katika hatua za mwisho na hivi karibuni itaingia sokoni.
[caption id="attachment_32246" align="aligncenter" width="600"] Mmoja ya watu wa karibu na Wema