Habari
Picha: Wema Sepetu na wenzake watua Central Polisi Dar kuitikia wito wa RC Makonda
Kufuatia agizo la mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kuwataka baadhi ya mastaa wanaoshukiwa kujihusisha na matumizi na biashara ya madawa ya kulevya kuwasili kituo cha polisi cha kati siku ya leo baadhi ya mastaa wametii agizo hilo na kuwasili.
Wema Sepetu akiwa Central Polisi
Malkia huyo wa filamu ambaye alikuwa mmoja kati ya wasanii waliotuhumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Da es salaam Paul Makonda kwamba anatumia Madawa ya kulevya, amewasili kituoni hapa nchana huu huku akiwa amevalia vazi hijab.
Wasanii wengine waliofika kituoni hapo ni pamoja na TID, Nyandu Tozzy pamoja na mtangazaji wa Clouds TV Babu wa Kitaa.
Mpaka sasa bado wanaendelea kuhojiwa.
Wema
TID akiwa kituoni hapo