Habari
Picha: Wolper Gambe na Ray kuigiza mke na mume kwenye filamu mpya
Waigizaji waliopo orodha A kwenye kiwanda cha filamu nchini, Vincent Kigosi aka Ray na Jacqueline Wolper aka Gambe, wapo location kushoot movie mpya. Kutokana na maelezo ya picha hizo walizoziweka kwenye akaunti zao za Instagram, inaonekana wanaigiza kama mke na mume.
“Siye tena kazini new movie, mke wa mtu me hapa nacheza.me en broo ray mwenyezi mungu kua nasi mwanzo hadi tumalize inshaalah ,” ameandika Wolper kwenye moja picha hizo.
Ray na Wolper on set
Wolper akipitia script.
Hata hivyo jina la filamu hiyo inayoandaliwa chini ya kampuni ya Ray, RJ Company haijajulikana inaitwaje.