Wema Sepetu
Picha ya Ommy Dimpoz na Wema Sepetu yazua mjadala mkubwa mtandaoni!
Waswahili wanasema kuwa ‘ushemeji huwa hausishi’.
Picha ya hitmaker wa ‘Ndagushima’ Ommy Dimpoz akiwa na ex wa Diamond Platnumz, Wema Sepetu imezua mjadala mkubwa kwenye mtandao wa Instagram.
Ommy amepost picha mbili tofauti kwenye akaunti yake ya Instagram akiwa na Wema anayeonekana akimrekebishia kitu kichwani kwake.
Muimbaji huyo hajaweka caption kwenye picha hiyo na hivyo kusababisha fumbo kubwa. Baadhi ya mashabiki wamehisi kuwa labda ushemeji kati ya wawili hao umeisha na sasa ni mtu na item wake.
“Jaman wa nyumban mbona mnachangia tena,” amehoji mmoja.
“I see you got a project number 2,” ameandika mwingine.
Mhh ukweli utajulikana tu!