Michezo

Picha: Yaliyojiri kwenye kesi ya Oscar Pistorius – Siku ya 2, shahidi wa pili asimulia kilichotokea, Oscar alia mahakamani

Kesi ya mwanariadha wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius Jumanne hii imeendelea kwa siku ya pili ambapo shahidi wa pili wa upande wa serikali amesema alisikia sauti za juu usiku alipouawa mwanamitindo Reeva Steenkamp.

article-2572735-1C06682000000578-460_634x426
Oscar akiwa ameziba masikio yake wakati ushahidi ukiendelea kutolewa

Kama alivyosema shahidi wa kwanza, Estelle van der Merwe anayeishi jirani na Pistorius ushahidi wake nao ulikinzana na maelezo ya mwanariadha huyo kuwa haikuwa ‘sahihi’ na sio sawa kusema kuwa alikuwa na ugomvi na mpenzi wake kabla hajafa. Van der Merwe ameiambia mahakama hiyo kuu ya North Gauteng mjini Pretoria kuwa alishindwa kulala mida ya saa 8 usiku kutokana na kelele za watu waliosikika wakigombana.

article-2572735-1C067DA600000578-415_634x417

Awali shahidi wa kwanza, Michelle Burger, alisema kuwa alisikia mwanamke akipiga kelele kuomba msaada, baadaye akasikia sauti ya mwanaume ikiomba msaada kabla ya milio ya bunduki kusikika. Katika hatua nyingine Oscar Pistorius alilia kwa uchungu mahakamani humo baada ya wakili wake kudai kuwa Reeva Steenkamp aliumia vibaya kwenye ubongo na hivyo haikuwa rahisi kupiga kelele.

Advocate Barry Roux alitoa maelezo hayo kufuatia ushahidi wa jirani yake aliyedai kusikia kelele baada ya milio ya bunduki.

article-2572735-1C06DE2C00000578-801_634x450

Hata hivyo kesi hiyo ilikatizwa katikati na jaji kuamuru kufanyika uchunguzi wa kwamba kituo kimoja cha runinga cha Afrika Kusini kilikuwa kikionesha picha za shahidi – kinyume na amri ya mahakama ya mashahidi kutooneshwa. Jaji Thokozile Masipa alivionya vyombo vya habari kuheshimu usiri wa mashahidi hao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents