Habari
Picha za Obama na mkewe alipo mtembelea Malkia kwenye ziara yake
Rais Obama na mkewe Michelle Obama jana alifanya ziara ya kutembelea nchi ya Uingereza na kufanikiwa kuonana na Malkia Elizabeth ambaye juzi alitimiza miaka 90 ya kuzaliwa.
Kwenye ziara hiyo Obama alitumia fursa ya kuishawishi nchi ya Uingereza isijiondoe kwenye umoja wa Ulaya kama ilivyopanga kufanya.
Akiongea baada ya mazungumzo na waziri mkuu wa Uingereza David Cameron mjini London, Obama alisema kuwa Uingereza itakuwa nyuma katika kuafikiana mikataba ya kibiashara na Marekani ikiwa itaondoka.
Hizi ni baadhi ya picha za Obama alipokutana na Malkia Elizabeth: