Pogba hana mpango na unahodha United ataka kutimkia Hispania
Nyota wa Manchester United, Paul Pogba anahitaji kuondoka ndani ya klabu hiyo na kuhamia kwa miamba ya soka ya Hispania Barcelona licha ya tofauti zake na Jose Mourinho kumalizika.
United imeendelea kusisitiza kuwa kiungo wake aliyesajiliwa kwa rekodi ya dunia pauni milioni 89 haitamuuza licha ya Pogba kuonesha dhamira yake ya kutimkia Hispania.
Meneja wa United, Mourinho anajaribu kumtuliza kiuongo huyo raia wa Ufaransa kwa kumpatia kitambaa cha unahodha ili kuhakikisha mambo yanakwenda sawa lakini baada ya mchezo wao wa kwanza wa ligi, Pogba amesema kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliyo fanyika mpaka kilakitu kitakapo anza kuwa sawa.
Hataivyo wakala wa Pogba, Mino Raiola anachaguo la kumuuza Barcelona au Real Madrid jambo United huenda ikaweka rekodi ya dunia katika mauzo yake.
Pogba mwenye umri wa miaka 25 alianzia kwenye mikono ya meneja Sir Alex Ferguson ndani ya United kisha kuuzwa katika klabu ya Juve mwaka 2012.
Akwendeeeee asituzingue
😒😒😒 tabu za nn za xaxa kama anataka aende tu kwan Man U bila Pogba inawezekana
safîiiiiiiiiiiii sanaaaasa?
C wamuache jamaaniii mnamfoc kwan ndo mwenye timu huyoo
Welcome
Chizi huyo