Habari

Polepole aguswa na jitihada za Doris Mollel kusaidia watoto njiti Tanzania (Video)

Kila tarehe 17 Novemba ni siku ya Mtoto Njiti Duniani ambapo wadau mbalimbali uungana kwa pamoja kuangalia namna gani watatua na kuweka mazingira rafiki ya kupunguza vifo vinavyotokana na mtoto kuzaliwa kabla ya muda wake.

Taasisi ya Doris Mollel Foundation chini ya Mkurugenzi wake @DorisMollel Jumanne hii katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar Es Salaam iliwakutanisha wadau mbalimbali kwaajili ya kujadili na kuangalia namna sahihi ya kuokoa maisha ya mtoto njiti ambao wako kwenye hatari kubwa ya kupoteza maisha kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Katibu Mwenezi chama cha Mapinduzi CCM comredi Hamphray Polepole alikuwa mgeni rasmi katika halfa hiyo ambapo katika mazungumzo yake alimpa kongole Doris Mollel pamoja na kuchukua changamoto zote za watoto njiti ili kwenda kuishauri serikali.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents